Vifo vya watu sita vimeripotiwa baada ya dhoruba ya Harvey kulikumba jimbo la Taxas Ijumaa usiku. Kikosi cha ulinzi wa pwani cha Marekani kimejitahidi kuwaokoa watu waliokwama baada ya maji kuendelea kufurika mjini Houston na maeneo ya karibu. Mpaka sasa kaunti 80 zimetangazwa kuathiriwa na maafa hayo, na viwanja viwili vikuu mjini Houston vimefungwa kutokana na mafuriko makubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |