• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Wafanyabiashara wa Soko la Sido wauzia bidhaa nje

    (GMT+08:00) 2017-08-29 20:38:53

    Wafanyabiashara wa Soko la Sido jijini Mbeya ambalo liliteketea kwa moto, wameamua kufanyia biashara nje ya soko hilo wakisubiri ruhusa ya kuanza ujenzi wa vibanda vya kudumu.

    Soko hilo liliungua moto usiku wa kuamkia Agosti 15 na kuteketeza mali za wafanyabiashara zenye thamani ya Sh14.29 bilioni, chanzo kikitajwa kuwa ni jiko la mkaa lililokuwa ndani ya moja vibanda sokoni hapo.

    Uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Mbeya umewaruhusu wafanyabiashara kuendelea na ujenzi wa vibanda vya kudumu kwa sharti la kufuata michoro maalumu.

    Leo baadhi ya wafanyabiashara wamepanga bidhaa kando mwa soko na wengine wakiuzia kwenye magari yao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako