Watoto 42 wamefariki dunia katika hospitali moja ya serikali katika jimbo la Uttar Pradesh kaskazini mwa India. Mkuu wa chuo cha matibabu cha Baba Raghav Das vilichotokea vifo hivyo Dk. P. K. Singh amesema kati ya watoto hao 42, saba walifariki kutokana na matatizo kwenye ubongo, na wengine walifariki kutokana na magonjwa mengine. Vyombo vya habari vya huko vimeripoti vifo vya watoto 61 katika hospitali hiyo ndani ya saa 72 zilizopita, ingawa havijathibitishwa rasmi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |