Polisi nchini Kenya wamesema watu watatu wameuawa baada ya magari waliyokuwa wanasafiria kushambuliwa na wanamgambo wasiojulikana, kwenye barabara kutoka Carsen hadi Lamu, mashariki mwa Kenya. Kamanda wa polisi kaunti ya Lamu Bw. Gilbert Kitiyo, amesema lori moja na gari moja dogo yalishambuliwa kwa mabomu na kufyatuliwa risasi na wanamgambo. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |