Kundi la waasi la zamani la Columbia Revolutionary Armed Forces of Colombia jana lilifanya mkutano na waandishi wa habari huko Bogoda likitangaza rasmi kuacha mapambano na serikali na kujiunga na mambo ya siasa, na kuunda chama cha FARC.
Kiongozi wa chama hicho Bw. Juan Manuel Santos Calderon alisema kuwa kifupi cha maandishi ya The Common Alternative Revolutionary Force kwa lugha ya Hispania FARC ni sawa na kifupi cha maandishi wa Revolutionary Armed Forces of Colombia, kufanya hivyo ni kwa ajili ya kuonesha urithi wa kundi hilo baada ya kuacha silaha na kujiunga na mambo ya siasa.
Chama hicho kilisema kuwa kinataka kuleta mabadiliko kwa jukwaa la siasa la Columbia, pia kiliwahimiza wanachama wengine wa kundi hilo waliokuwa na maoni ya tofauti kwa makubaliano ya amani wajisalimishe na kujiunga na jamii tena.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |