Mkutano wa tisa wa viongozi wa nchi za BRICS yaani Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini umefunguliwa leo mjini Xiamen, China.
Rais Xi Jinping wa China ameendesha mkutano huo unaohudhuriwa na waziri mkuu wa India Bw Narendra Modi, rais Jocob Zuma wa Afrika Kusini, rais Michel Temer wa Brazil na rais Vladimir Putin wa Russia.
Kwenye mkutano huo, viongozi wa nchi hizo tano wanatarajiwa kujadili hali ya uchumi wa dunia, usimamizi wa uchumi wa dunia na masuala ya kimataifa na ya kikanda, na kupitisha "Azimio la Xiamen".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |