Jeshi la Syria limesema, makamanda wa kigeni wa Kundi la IS wamekimbia mapambano kati ya kundi hilo na jeshi la serikali, linalolenga kuwaondoa wapiganaji wa IS wanaozingira mji wa Deir al-Zour, mashariki mwa Syria.
Vikosi vya Syria jana vimewashambulia kutoka pande mbili ili kumaliza kuzingirwa kwa kambi ya Brigedi ya 137 ya jeshi la serikali iliyoko magharibi mwa mji wa Deir al-Zour, ambako karibu askari elfu tano wa Syria wamezingirwa katika kambi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |