• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yatangaza tarehe ya kufanya upya uchaguzi wa urais

    (GMT+08:00) 2017-09-05 10:15:27

    Tume ya Uchaguzi Mipaka ya Kenya IEBC jana imetangaza kuwa, uchaguzi wa urais utafanyika tena tarehe 17 Oktoba, baada ya Mahakama Kuu ya Kenya kuamua kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika Agosti 8.

    Mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati amesema kiongozi wa upinzani Raila Odinga na rais Uhuru Kenyatta watakuwa wagombea pekee katika uchaguzi huo.

    Pia Chebukati amesema tume hiyo inapitia upya matakwa ya utekelezaji na utaratibu wa uchaguzi mpya, na itawafahamisha wahusika mapema iwezekanavyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako