Rais Xi Jinping wa China amesema, viongozi wa nchi tano za BRICS wamekubaliana kuwa, nchi za BRICS zenye nguvu ya ushawishi zinapaswa kuimarisha mawasiliano na uratibu katika masuala muhimu duniani, na kuhimiza uanzishwaji wa utaratibu mwafaka na ulio wa haki zaidi wa kimataifa. Pia zinapaswa kuonesha kazi ya kiujenzi katika kulinda kanuni za kimsingi za uhusiano wa kimataifa na kulinda usawa na haki duniani. Rais Xi pia amesisitiza umuhimu wa kuongeza sauti za nchi zinazoibuka kiuchumi na nchi zinazoendelea duniani, ili kuweka mazingira mazuri zaidi kwa maendeleo ya nchi hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |