Mipango ya kuanzisha kiwanda cha magari cha kampuni ya Volkswagen nchini Rwanda (VW) iko karibu kukamilika.
Mwenye kiti wa Volkswagen nchini Afrika Kusini Thomas Schäfer, amesma kampuni hiyo ya Ujerumani inapanga kuanza oparesheni Rwanda kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Schäfer amesema kiwanda cha Rwanda kitaanza kwanza kutengeneza magari 1,000 kwa mwaka na kuongezea kulingana na mahitaji.
Desemba mwaka jana VolksWagen ilitia saini makubaliano na serikali ya Rwanda na kampouni hiyo kufanya utafiti ambao umebaini kuna mazingira mazuri ya kuwekeza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |