Ripoti iliyotolewa na ofisi ya kamishna mwandamizi wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa inasema, zaidi ya raia elfu tano, wakiwemo watoto zaidi ya elfu moja, wameuawa kwenye mapigano yaliyoanza mwanzoni mwa mwaka 2015 nchini Yemen. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mashambulizi ya anga yaliyofanywa na jeshi la muungano linaloongozwa na Saudi Arabia, ni chanzo kikubwa zaidi cha vifo vya raia, na kwamba hivi sasa watu milioni 19 kati ya jumla ya milioni 27 nchini humo, wanahitaji misaada ya kibinadamu, na milioni 7.3 kati yao wanakabiliwa na hatari ya njaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |