Ripoti iliyotolewa na Benki ya Dunia imesema ukuaji wa uchumi wa Rwanda ulipungua kuanzia katikati ya mwaka jana, hivyo kukua kwa asilimia mwaka jana, na asilimia 4.2 katika robo ya kwanza ya mwaka huu, lakini uchumi wa nchi hiyo unakadiriwa kuanza tena kukua kwa kasi katika nusu ya pili ya mwaka huu.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa leo mjini Kigali, imesema kushuka kwa uchumi kulisababishwa na ukame, bei ya chini ya usafirishaji, na vitendo vya ujenzi kutokana na kumalizika kwa miradi mikubwa ya uwekezaji mwaka jana. Pia ripoti hiyo imesema sera ya uchumi wa mazingira katika mwaka 2017 imeboreshwa na mfumuko wa bei umeshuka na kufikia chini ya asilimia 5 mwezi Juni, ikiwa ni chini kutoka kiwango cha juu cha asilimia 8 mwezi Februari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |