• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ujumbe wa Umoja wa Ulaya watetea nafasi ya usimamizi katika uchaguzi wa rais nchini Kenya
     

    (GMT+08:00) 2017-09-06 19:20:07
    Umoja wa Ulaya umetetea nafasi yake katika uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8 nchini Kenya ambao matokeo yake yamefutwa na Mahakama Kuu ya nchi hiyo wiki iliyopita.

    Kiongozi wa Tume ya kusimamia uchaguzi ya Umoja wa Ulaya nchini Kenya Marietje Schaake amesema kuwa kazi yao ilikabiliwa na changamoto kutokana na teknolojia iliyotumiwa na tume ya uchaguzi. Amesema uchaguzi wa Kenya ulitegemea kwa kiasi kikubwa kampuni binafsi na mifumo yao, hivyo haikuwa rahisi kwao kuelewa jinsi mifumo hiyo inavyofanya kazi.

    Schaake amesema hayo baada ya Wakenya kuikosoa tume hiyo ya kimataifa kwa kuthibitisha kuwa mchakato wa uchaguzi ulikuwa huru, haki na wa wazi, licha ya makosa yaliyoonekana kwenye mchakato huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako