Polisi nchini Kenya imethibitisha kuwa wapiganaji wanaotuhumiwa kutoka kundi la Al-Shabaab jana usiku wamewachinja watu wanne katika kaunti ya Lamu nchini Kenya.
Kamada wa polisi wa kanda ya Pwani Larry Kieng amesema, wanakijiji wanne walipigwa risasi kisha kukatwa vichwa na wapiganaji wenye silaha walioshambulia kijiji cha Hindi.
Kieng amesema, maofisa usalama wanawasaka watuhumiwa ambao walikimbilia msitu wa Boni ambao wanautumia kama sehemu yao ya kujificha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |