• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mcheza tenis wa Afrika Kusini atinga hatua ya nusu fainali Michuano ya wazi ya Marekani

    (GMT+08:00) 2017-09-07 08:26:28

    Mcheza tenis raia wa Afrika Kusini, Kevin Anderson amefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya wazi ya Marekani 'US Open' baada ya kumshinda mpinzani wake, Sam Querrey. Anderson amefanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kumshinda Mmarekani, Sam Querrey kwa jumla ya seti 7-6 (7-5) 6-7 (9-11) 6-3 7-6 (9-7) mchezo uliopigwa katika viwanja vya Flushing Meadows siku ya Jumanne.

    Kevin Anderson mwenye umri wa miaka 31 amekuwa muafrika kusini wa kwanza kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano mikubwa ya Grand Slam tangu alivyoweza kufanya hivyo mcheza tenis, Wayne Ferreira mwaka 2003 katika michuano ya Australian Open.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako