Timu ya taifa ya Uturuki ya mpira wa kikapu imeichapa Ubelgiji kwa pointi 78-65 katika mashindano ya Ulaya ya mwaka 2017. Katika mechi ya nne ya kundi D, timu ya Uturuki imeshinda mara mbili na kupelekea kupata matumaini ya kuendelea kwenye mzunguko wa mwisho wa 16.
Baada ya mechi ya nne, Urusi, Serbia, Lativia na Uturuki zimejumuishwa katika mzunguko wa mwisho wa 16, huku Ubelgiji na Uingereza zikiaga mashindano. Timu ya Uturuki itakutana na Latvia siku ya Alhamisi Septemba 7 katika mechi ya mwisho ya kundi D.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |