• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza la Usalama lalaani shambulizi dhidi ya jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa nchini Mali

    (GMT+08:00) 2017-09-07 19:22:15

    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetoa taarifa kulaani vikali shambulizi dhidi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Mali, ambalo limesababisha vifo vya walinzi wawili wa amani kutoka Chad na wengine wawili kujeruhiwa katika sehemu ya Kidal nchini Mali.

    Taarifa hiyo imesema, wajumbe wa baraza hilo wanatoa salamu za rambirambi kwa jamaa wa walinzi waliouawa, serikali ya Chad na ujumbe huo, kuwatakia majeruhi wapone haraka na kutoa heshima kwa walinzi wa amani walio hatarini nchini Mali.

    Taarifa hiyo pia imesema, wajumbe wa baraza hilo wanaitaka serikali ya Mali kufanya uchunguzi kuhusu shambulizi hilo na kuwakamata washambuliaji.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako