Mahakama ya kikatiba nchini Hispania imesitisha ombi la kura za maoni kwenye eneo la Catalonia mashariki mwa nchi hiyo, baada ya serikali ya Hispania kuitaka mahakama hiyo kuzuia ombi hilo lililopitishwa kwenye bunge la kikanda na kuamua kupiga kura za maoni Oktoba mosi. Mahakama hiyo pia imezionya serikali 947 za mitaa kwenye eneo la Catalonia na maofisa 62 wa serikali ya eneo hilo, kutoshiriki kwenye maandalizi ya kura hizo za maoni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |