Idadi ya watu waliofariki kutokana na tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 8.2 kwenye kipimo cha Richter lililotokea Alhamisi nchini Mexico, imefikia 90. Gavana wa jimbo la Oaxaca lililoathiriwa vibaya na tetemeko hilo Bw. Alejandero Murat, amesema tetemeko hilo limesababisha vifo vya watu 71 na kuwaathiri watu wengine laki nane. Bw. Murat amesema hivi sasa kazi za uokoaji bado zinaendelea na idadi ya wahanga huenda ikaongezeka zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |