Polisi nchini Cyprus wamesema wakimbizi 305 wa Syria wakiwemo wanawake 30 na watoto 73, walifika nchini humo jumamosi kwa meli mbili. Msemaji wa polisi ya Cyprus amesema meli hizo zilizojaa watu kupita kiasi ziligunduliwa kwenye bahari ya kaskazini magharibi mwa nchi hiyo, na serikali ya Cyprus ilituma meli kadhaa na helikopta moja kuwaokoa. Msemaji huyo amesema wakimbizi wapatao 800 kutoka Syria wamefika Cyprus kwa njia ya bahari mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |