Mamlaka nchini Iraq zinawashikilia wanafamilia 1,400 wa wapiganaji wa kigeni wa kundi la Islamic State kwenye kambi moja karibu na mji wa Mosul uliokombolewa hivi karibuni, kaskazini mwa nchi hiyo. Naibu katibu wa waziri anayeshughulikia masuala ya wakimbizi na uhamiaji wa Iraq Bw. Jasim al-Attiyah amesema vikosi vya usalama vinawahoji watu hao waliozuiliwa huko Hammam al-Alil, ili kuthibitisha uraia wao kwa kuwa wengi wao hawana hati za za asili za kujitambulisha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |