Wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ikisema, Korea Kaskazini itachukua hatua dhidi ya Marekani kama ikiendelea kutoa pendekezo jipya la vikwazo dhidi yake katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Taarifa hiyo imesema, kitendo cha Korea Kaskazini kufanya utafiti wa silaha za nyuklia ni hatua ya kukabiliana na tishio la kinyuklia la Marekani dhidi ya nchi yake na kwamba ni kitendo halali cha kujilinda.
Habari zinasema, leo Marekani inapanga kuidhinisha mswada mpya wa vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini na kutarajia kupiga kura kwenye baraza hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |