Rwanda imepoteza mchezo wake mikononi mwa Cameroon kwa kukubali kichapo cha 77-81 na kukosa nafasi ya kucheza robo fainali za michuano ya 29 ya ubingwa wa mpira wa kikapu barani Afrika (Afrobasket) Rwanda ilianza mchezo kwa nia kushinda na ilitawala robo ya kwanza kwa kuongoza kwa magoli 22-18. Hata hivyo, mambo yalibadilishwa haraka na Cameroon hadi wakati wa mapumziko Cameroon ilikuwa ikiongoza kwa 41-36. Mwisho wa mchezo Cameroon waliibuka kwa ushindi wa 81-77 dhidi ya Rwanda, huku Egypt ikiifunga Afrika Kusini 70-51
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |