Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa mataifa UNHCR limesema makazi elfu 40 zaidi yanahitajika kuwapokea wakimbizi katika nchi 15 zlizo kwenye njia ya Mediterranean ya kati. Kamishna mwandamizi wa shirika hilo Bw Filippo Grandi amesema makazi hayo ni muhimu kuwasaidia wakimbizi wenye mahitaji zaidi kwenye kanda ya Mediterranean ya kati, na mpaka sasa ni wakimbizi 6,700 tu walioko kwenye njia hiyo kuelekea Libya wamepewa makazi mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |