Michuano ya klabu bingwa barani ulaya kwa msimu wa 2017/2018 utaanza rasmi leo kwa jumla ya michezo 8 kwenye viwanja mbalimbali.
Kundi A, Manchester United watakuwa nyumbani uwanja wa Old Trafford wakiwakaribisha wabelgiji wa Anderlecht, bao Celtic wataanza kibarua kizito dhidi ya PSG.
Chelsea wataanza safari ya kuwania ubingwa huo kwa kuwakaribisha Qarabag FK, na AS Roma wao wataanza na Atletico Madrid ikiwa ni michezo ya kundi C.
Barcelona watakuwa kwenye dimba lao la Nou Camp kukipiga na vibibi vizee vya Juventus, Olympiacos ya Ugiriki watakutana na Sporting CP ya Ureno.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |