Kampuni ya televisheni ya China StarTimes inapanga kuzindua huduma za matangazo ya TV ya kidijitali bila malipo kwenye sehemu za vijijini barani Afrika, ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kijamii.
Mkurugenzi Masoko na Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Japheth Akhulia amesema mradi huo utanufaisha vijiji 10,000 barani Afrika. Kwa sasa StarTimes imekuwa sehemu muhimu ya jamii ya Afrika, na hivyo inahitaji kuchangia katika kuendeleza jamii kwa kuboresha hali yao ya maisha.
Hivi sasa StarTimes inafanya mazungumzo na maofisa wa serikali za nchi mbalimbali za Afrika ili kutafuta njia ya kuhakikisha utekelezaji wa mradi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |