Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) limetoa ripoti ya hali ya maisha ya watoto katika nchi zinazokumbwa na mapigano za Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini na kutoa wito kuharakisha kusimamisha mapambano na kutoa misaada ya dharura.
Ripoti hiyo imesema kutokana na mapambano, ukosefu wa matibabu na maji safi, asilimia 20 ya watoto wa maeneo hayo wanahitaji msaada wa dharura.
Ripoti hiyo pia imesema watoto wengi wa huko wanafanya kazi au kuolewa katika umri mdogo kutokana na mapato machache ya familia. Pia idadi ya askari watoto inaongezeka kwa kasi.
Mkurugenzi wa UNICEF katika eneo hilo Bw Geert Cappelaere amesema, mapambano hayo yanawafanya maelfu ya watoto kupoteza utoto wao
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |