Ujenzi wa mradi wa kuzalisha kawi wa Nyabarongo katika eneo la maghribi mwa Rwanda utasaidia upatikanaji wa kawi kwa watu zaidi nchini humo.
Mradi huo ambao ndio mkubwa zaidi wa kawi ya maji nchini Rwanda utachangia zaidi ya megawati 28 kwenye gridi ya taifa.
Mradi huo umetekelezwa kwa ushirikiano wa mashirika ya Angelique International, Bharat Heavy Electrical Limited (BHEL) na serikali ambayo ilitoa dola milioni 110.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |