• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Mashirika 20 ya ndege yakubalia Kenya

    (GMT+08:00) 2017-09-12 18:50:46

    Mamlaka ya usafiri wa anga nchini Kenya (KCAA) imeidhinisha mashirik aya ndege 20 kutoka Ulaya na Afrika kuanza safari za moja kwa moja kuingia Kenya,

    KCAA imesema ilifanya utafiti na kutosheka kuwa mashirika hayo yanatimiza viwango vyote kupewa leseni za kusafirisha abiria na shehena.

    Sasa mamlaka hiyo imetoa siku 21 kwa wadau kwenye sekta ya usafiri wa anga kutoa maoni yao kuhusu athari zozote za kuruhusu mashirika hayo kuhudumu Kenya.

    Miongoni mwa mashirika yalioruhusiwa kuhudumu Kenya kutoka nchi za Afrika ni kama vile East African Air Charters, Exclusive Air Services, AIMAir, Ventura Aviation na Kasas.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako