Bingwa wa mbio za marathoni za London, Mary Keitany ameshinda tena mbio za Great North kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kutumia muda wa 1:05:59 nchini Uingereza. Keitany alikamilisha mbio hizo za kilomita 21 mbele ya mwenzake Vivian Cheruiyot na Catherine Kiprikui alimaliza wa 3. Mbio hizo zilianzia Newcastle na kukamilika mjini South Shields zilishirikisha jumla ya wanariadha 12,000 duniani kote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |