Naibu katibu wa wizara ya mambo ya kibinadamu na usimamizi wa majanga ya Sudan Kusini Bw. Gatwech Kulang amesema zaidi ya watu laki moja wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa katika mwezi uliopita kwenye sehemu za kati na kaskazini mwa nchi hiyo. Bw. Kulang amesema mafuriko yanaweza kuifanya hali ya kibinadamu nchini humo izidi kuwa mbaya, na kutoa wito kwa mashirika ya kibinadamu kushirikiana na serikali ya Sudan Kusini katika kukabiliana na hali hiyo ya dharura.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |