Bunge la Iraq limepitisha azimio la kupinga upigaji kura za maoni wa jimbo la wakurd utakaofanyika hivi karibuni.
Habari zinasema azimio hilo limetoa mwito kwa waziri mkuu wa Iraq Bw Haider al-Abad achukue hatua zote kulinda umoja wa taifa, na kufanya mazungumzo na jimbo la wakurd, ili kutatua masuala kati ya serikali ya Iraq na jimbo linalojitawala la Kirkuk.
Konsela wa mwenyekiti wa jimbo la wakurd akiwa ni waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Iraq Bw Hoshyar Zebari amesema upigaji kura za maoni utafanyika kama ilivyopangwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |