Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa imechagua mji mkuu wa ufaransa, Paris, kuwa mwenyeji wa michuano ya Olimpiki mwaka 2024, na kuutunuku mji wa Los Angeles nchini Marekani kuwa mwenyeji wa michuano hiyo mwaka 2028. Mwezi uliopita, kamati hiyo ilifanya maamuzi ya kuwa Olimpiki mbili za majira ya joto zitatolewa kwa wakati mmoja, baada ya miji kadhaa kuahirisha zabuni zao kutokana na wasiwasi wao kuhusu ukubwa, gharama, na utata wa kuandaa moja ya matukio makubwa kama hayo ya michezo duniani. Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema mji wa Paris kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ni ishara ya kutambuliwa kwa mji na nchi kitu ambacho kila Mfaransa anapaswa kusherehekea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |