Bondia Floyd Mayweather kwa sasa anafurahia kwa kufanikiwa kulinda rekodi yake ya kutopoteza pambano hata moja katika mapambano yake 50 baada ya kufanikiwa kumpiga Bondia Mc Gregor kwa Technical Knock Out (TKO) round ya 10 katika pambani la round 12. Mayweather ameripotiwa na mtandao wa dailymail.co.uk kuwa pambano lake na Mc Gregor ndio pambano lake la mwisho na ameamua kustaafu mchezo wa ngumi, japokuwa kuna watu wanaweza kufikiria kuwa atarudi tena ulingoni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |