Naibu mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Afrika Bw. Thomas Kwesi Quartey, ameipongeza serikali ya Ghana kutokana na sera yake ya kutoa elimu ya sekondari ya juu bila malipo. Akiongea mjini Geneva kwenye mkutano wa ngazi ya juu ulioandaliwa na Shirika la biashara na maendeleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD, Bw. Quartey amesema hii ni njia ya kuhakikisha maendeleo ya Ghana na Afrika kwa ujumla, na kwamba sera ya elimu ya bila malipo itatoa msukumo mkubwa kwa ajenda ya Umoja wa Afrika, ya kuhakikisha kila mtoto wa Afrika anapata elimu kabla ya mwisho wa muongo huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |