Bandari ya Mombasa nchini Kenya imeshuhudia ongezeko la asilimia 11.9 la mizigo katika miezi 7 ya mwanzo ya mwaka huu, ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hicho. Mkurugenzi wa mamlaka ya bandari Kenya Bibi Catherine Mturi-Wairi amesema kuanzia mwezi Januari hadi Julai mwaka huu, bandari hiyo ilipitisha tani milioni 17.52 za mizigo, kiasi ambacho kimeongezeka kutoka tani milioni 15.66 za mwaka jana wakati kama huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |