Kundi la Houthi la Yemen limemshutumu aliyekuwa rais wa nchi hiyo Bw. Ali Abdullah Saleh kwa kuiunga mkono Saudi Arabia, na kutishia kujitoa kwenye muungano wa kisiasa na kijeshi na Bw. Saleh. Taarifa iliyotolewa jana na kundi hilo inasema, chama cha GPC kinachoongozwa na Bw. Saleh kimeonesha msimamo wazi wa kuwaunga mkono maadui, kwa hivyo sio heshima kuendelea kushirikiana nacho kwenye mambo ya taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |