Mjumbe wa taifa wa China Bw. Yang Jiechi amekutana na msaidizi wa rais wa Marekani anayeshughulikia mambo ya usalama Bw. H. R. McMaster na mshauri mwandamizi wa rais Bw. Jared Kushner kwenye Ikulu ya Marekani.
Pande hizo mbili zimekubali kuimarisha mawasiliano ya ngazi mbalimbali, kupanua ushirikiano, kufanya maandalizi ya ziara ya kiserikali ya rais Donald Trump nchini China itakayofanyika mwishoni mwa mwaka huu, na kusukuma mbele maendeleo mazuri ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |