Kampuni ya kutengeneza rangi ya AkzoNobel kutoka uholanzi imefuta makubliano yake na ile ya Sadolin Paints East Africa.
Sadolin imekuwa ikiendesha oparesheni zake chini ya jina Kansai Plascon.
AkzoNobel imesema ilifuta leseni na makubaliano hayo kutokana na ukiukaji mkubwa wa mkataba,
Hii inamaanisha sasa kampuni ya Kansai Plascon ambayo ilikuwa imenunua Sadolin haitatengeneza au kuuza rangi Sadolin kama ilivyokuwa imekubaliwa hadi mwaka 2018.
Mkurugenzi mkuu wa AkzoNobel bwana Johann Smidt, amesema kampuni yake imefanya majaribio kaddhaa Kansai Plascon kuendelea kuzalisha mfululizo bidhaa za sadolin lakini hawajatimiza matakwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |