Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limepitisha azimio la kurefusha muda tume ya Umoja huo nchini Libya hadi Septemba 15 mwaka kesho. Azimio hilo linaitaka tume hiyo isaidie kusukuma mbele mchakato shirikishi wa kisiasa chini ya mfumo wa Makubaliano ya kisiasa ya Libya, kuhimiza utekelezaji wa makubaliano hayo, na kuisaidia serikali ya maafikiano ya Libya kuimarisha utawala wa nchi, kujenga uwezo wa kulinda usalama na kuendeleza uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |