Ofisa habari wa rais wa Russia Bw. Dmitry Peskov amesema hivi karibuni miji kadhaa mikubwa ya Russia ilisumbuliwa kwa mfululizo na ripoti feki za simu kuhusu matishio ya mabomu, na kuvitaja vitendo hivyo kuwa ugaidi kwa njia ya simu. Bw. Peskov amesema uchunguzi kuhusu vitendo hivyo vya kigaidi kwa njia ya simu unaendelea. Habari kutoka Russia zinasema katika siku tatu zilizopita, ripoti feki za mabomu zilihusisha sehemu 500 za umma nchini Russia na kusababisha watu wengi kuondolewa kutoka kwenye sehemu hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |