Waziri wa fedha wa Uingereza Bw. Philip Hammond amesema jukumu lake kuu ni kuhakikisha Uingereza inaendelea kuwa kituo cha kifedha duniani baada ya kujitoa Umoja wa Ulaya. Bw. Hammond amesema sekta ya huduma za kifedha ikiwa ni sekta muhimu ya nchi hiyo katika Umoja wa Ulaya, inapaswa kulindwa. Pia amesema anaelewa wasiwasi wa Umoja wa Ulaya kuhusu usimamizi wa mashirika ya kifedha yenye makao makuu mjini London yanayotoa huduma za kifedha kwa nchi za Ulaya, na kusisitiza kuwa Uingereza haitatekeleza "sera ya kujilinda kwa kisingizio cha usalama wa kifedha".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |