Askari 15 walijeruhiwa kutokana na mlipuko uliotokea wakati wanapewa mafunzo katika kituo cha kijeshi cha Fort Bragg, jimbo la Carolina Kaskazini nchini Marekani. Maofisa wa kituo hicho wamesema mlipuko huo ulitokea baada ya gari moja kupinduka ndani ya kituo hicho, na waliojeruhiwa wote ni makamando wa kikosi maalumu. Uchunguzi kuhusu tukio hilo bado unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |