• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa laitisha mkutano wa dharura kujadiliana majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini

    (GMT+08:00) 2017-09-15 17:42:21
    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litafanya mkutano wa dharura kutokana na ombi la balozi wa Marekani na Japan katika Umoja huo ili kujadili kuhusu Korea Kaskazini kufanya majaribio mapya ya makombora.

    Makao makuu ya jeshi la Marekani ya kanda ya pasifiki limesema, jana usiku Korea Kaskazini ilirusha makombora yaliyopita anga ya Japan na kuanguka katika bahari ya Pasifiki.

    Serikali ya Japan ilithibitisha taarifa hiyo na kulaani vikali kitendo hicho cha Korea Kaskazini.

    Wakati huohuo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Hua Chunying amesema China inapinga jaribio la kombola lililofanywa na Korea Kaskazini ambalo limekwenda kinyume na maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako