Shirika la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD limetoa ripoti ikizihimiza serikali za nchi mbalimbali kuondoa sera za kubana matumizi, ili kusukuma mbele kazi ya kufufua uchumi wa dunia.
Kwenye ripoti ya biashara na maendeleo ya 2017, Shirika hilo limesema inakadiriwa kuwa ongezeko la uchumi wa dunia la mwaka huu ni asilimia 2.6, ingawa ni kubwa zaidi kuliko mwaka jana ambalo lilikuwa asilimia 2.2, lakini bado ni dogo zaidi kuliko ongezeko la wastani kati ya mwaka 2001 hadi 2008 ambalo ni asilimia 3.2
Ripoti hiyo inasema sababu kuu inayozuia kufufuka kwa uchumi ni sera za kubana matumizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |