Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China bibi Hua Chunying amesema China inaitaka Uingereza isiingilie mambo ya China.
Hivi karibuni serikali ya Uingereza ilitoa ripoti ya nusu mwaka ya suala la Hongkong. Msemaji huyu alipozumguzia jambo hili amesema serikali ya China ilirudisha mamlaka kwa Hongkong tarehe 1 mwezi Julai mwaka 1997, hivyo mambo ya Hongkong ni mambo ya ndani ya China, na China inaitaka Uingereza isiingilia mambo hayo na kutotoa ripoti husika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |