Mahakama kuu ya Misri -Jumamosi ilimhukumu rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi kifungo cha maisha kwa uhalifu wa kuvujisha siri ya taifa kwa Qatar.
Taarifa ilisema kuwa, mahakama kuu ya Misri ilimhukumu Morsi kuvujisha nyaraka ya siri kuhusu usalama wa taifa wa Misri na upangaji wa jeshi wa Misri kwa Qatar, na kumhukumu kifungo cha miaka 25 na haimruhusu kukata rufaa. Kutokana na sheria ya Misri, kifungo cha miaka 25 ni sawa na kifungo cha maisha.
Aidha, wanachama 3 wa kundi la Muslim Brotherhood walihukumiwa adhabu ya kifo kwa uhalifu huo pia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |