Timu ya wavulana wa volleyball ya Rwanda itaanza maandalizi jumatano hii kwa ajili ya mashindano ya kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2017 na michuano ya kufuzu kucheza kombe la dunia ya volleyball kwa wanaume mwaka 2018 itakayoanza Oktoba 20-30 nchini Tunisia.
Rwanda imekamilisha nafasi ya pili nyuma ya Kenya katika mashindano ya kufuzu kucheza kombe la mataifa ya Afrika yaliyofanyika mwezi uliopita nchini Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |