Al Hilal ilianza kupata bao katika dakika za mwanzo za mchezo huo kupitia kwa Mohamed Tahir kabla ya Malango kuisawazishia Mazembe na kwenda mapumziko bao 1-1, kipindi cha pili dakika ya 83 Malango aliipatia bao la ushindi Mazembe.
Katika robo fainali nyingine FUS Rabat walitoka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Cs Sfaxien. MC Alger nao wakiwa nyumbani waliichakaza Club African bao 1-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |