Jeshi la Iraq limesema mashambulizi ya anga yaliyofanywa dhidi ya kundi la Islamic State kwenye maeneo ya magharibi mwa Iraq, yameharibu vituo vingi vya kundi hilo na kuwaangamiza wapiganaji 306. Kabla ya hapo, vikosi vya usalama vya Iraq vilifanikiwa kuwaondoa wapiganaji wa kundi hilo kutoka miji ya Ramadi na Fallujah, lakini maeneo yaliyoko karibu na mpaka wa Syria na maeneo ya vijijini mkoani humo bado yanadhibitiwa na kundi la IS.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |